Jamhuri ya China

Nchi za Asia Mashariki
Makala hii yaeleza habari za Taiwan. Kwa habari za Jamhuri ya Watu wa China au China bara tazama hapa


Jamhuri ya China (pia: Taiwan) ni nchi ya visiwani katika Asia ya Mashariki upande wa kusini-mashariki wa China bara.

Jamhuri ya China
中華民國
Zhōnghuá Mínguó
Bendera ya Taiwan Nembo ya Taiwan
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Misingi mitatu ya taifa
(三民主義 San-min Chu-i)
Wimbo wa taifa: Wimbo la taifa la Jamhuri ya China
Lokeshen ya Taiwan
Mji mkuu Taipei (hali halisi)1 
25°02′ N 121°38′ E
Mji mkubwa nchini Taipei
Lugha rasmi Kichina (Guóyǔ)
Serikali
Rais
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya China
Waziri Mkuu
Demokrasia
Tsai Ing-wen
Chen Chien-jen
Su Tseng-chang
Tarehe za Kihistoria
Jamhuri ilitangazwa
Iliundwa
Ilihamia
   Taiwan

10 Oktoba 1911
1 Januari 1912
7 Desemba 1949
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
36,193 km² (136)
10.3
Idadi ya watu
 - 2018 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
23,780,452 (ya 532)
650/km² (ya 172)
Fedha Dollar mpya ya Taiwan (NT$) (TWD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CST (UTC+8)
not observed (UTC)
Intaneti TLD .tw
Kodi ya simu +886

-

1 Serikali ya Kuomintang ilitaja mji wa Nanking (China bara) kama mji mkuu rasmi
2 takwimu za 2006


Eneo hariri

Sehemu kubwa ya eneo lililo chini ya serikali ya Jamhuri ya China ni kisiwa cha Taiwan, lakini pia lina visiwa vidogo mbele ya mwambao wa China bara.

Mbali ya visiwa mbalimbali katika Bahari ya China visivyo na wakazi, upande wa magharibi kuna mafunguvisiwa matatu:

Historia hariri

Jamhuri ya China iliundwa mwaka 1912 mjini Nanking baada ya mapinduzi ya China ya 1911 iliyomaliza utawala wa kifalme wa nasaba ya Qing. Sun Yat-sen akawa rais wa kwanza.

Serikali ya jamhuri ilidai mamlaka juu ya China yote ingawa hali halisi viongozi wa kijeshi na wapinzani mbalimbali walishika utawala katika maeneo kadhaa.

Nchi jinsi ilivyo sasa ni tokeo la vita vya wenyewe kwa wenyewe vya China iliyokwisha mwaka 1949 na ushindi wa Wakomunisti chini ya Mao Zedong na kuundwa kwa Jamhuri ya Watu wa China huko Beijing.

Wakomunisti walifukuza serikali ya chama cha Kuomintang iliyoongoza Jamhuri ya China.

Mwaka 1949 serikali ya Kuomintang chini ya jenerali Chiang Kai-shek na mabaki ya jeshi lake pamoja na wafuasi wengi ilihamia Taiwan walipoendelea kutawala. Wakomunisti walikosa nguvu ya kuwafuata hadi kwenye visiwa kutokana na vitisho vya Marekani.

Hivyo serikali katika Taiwan iliendelea kujiita "serikali ya China" na kutangaza shabaha yake kuwa ukombozi wa China yote.

Hali halisi utawala wa Wakomunisti barani uliimarika na mipango yote kinyume chake ilionekana kama ndoto. Lakini kwa miaka minghi serikali ya Taipeh ilichukua nafasi ya China yote kimataifa.

Jamhuri ya China ilikuwa kati ya nchi zilizoanzisha Umoja wa Mataifa mwaka 1945 na serikali ya Kuomintang iliendelea kushika kiti cha China hadi mwaka 1971.

Tarehe 25 Oktoba 1971 Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa uliamua ya kuwa Jamhuri ya Watu wa China iwe mwakilishi wa China bara kwenye UM, hivyo Jamhuri ya China alijiondoa.

Siku hizi uhusiano kati ya China zote mbili ni mgumu. Wananchi wengi wa Jamhuri ya China wameanza kujitazama kama Wataiwani, si Wachina tena. Lakini China inadai nchi hii ni sehemu yake.

Nchi imefaulu sana kiuchumi, ikishika nafasi ya 15 duniani.

Watu hariri

Wakazi ni 23,780,452 (2018), hivyo msongamano ni mkubwa sana.

Wengi wao (zaidi ya 95%) ni Wachina waliotokana na wale waliohamia kisiwani hasa kuanzia karne ya 17. Wenyeji ni 2% tu.

Kichina ndiyo lugha rasmi na ya taifa, pia lugha ya kawaida katika lahaja zake mbalimbali. Lugha za wenyeji, ambazo ni kati ya lugha za Austronesia, zinazidi kufa.

Nchi inaheshimu uhuru wa dini na wakazi wengi (81.3%) wanayo moja ya kwao. Serikali inazitambua 26.

Yenye wafuasi wengi ni Ubuddha (35.1%), Utao (33%), Ukristo (3.9%, wakiwemo Waprotestanti 2.6% na Wakatoliki 1.3%) na Yiguandao (3.5). Wenyeji wengi ni Wakristo (64%).

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons

Taarifa za jumla hariri

Serikali hariri

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


  Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Jamhuri ya China kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.